kukombolewa ktk nafsi


Nilikuwa ninafanya huduma sehemu fulani ndipo akanijia ndugu mmoja na kuniambia kuwa anahitaji msaada wangu. Nikaaanza kujitetea, maana hapo mahali nilikuwa nikitumika chini ya mtumishi mwingine, aliyekuwa anaiongoza hiyo huduma. Mpendwa huyu alinisihi sana kiasi nikaguswa ikabidi nimsikilize.

Mpendwa huyu alikuwa ni mama mmoja aliyeteseka sana katika maisha yake bila kujua tatizo ni nini na akiishia kwenda kwenye maombi kwa miaka mingi sehemu mbalimbali bila mafanikio. Ndipo aliponijia na kunieleza, “mtumishi naomba uniombee.” Nikamwuliza nikuombee nini? Kwa kuwa yeye alikuwa muwazi, akanambia mtumishi mimi naona Mungu hajibu maombi yangu.

 

Nilimhoji mama huyu mambo fulani fulani lakini niligundua katika mahojiano naye anabidii ya kwenda kanisani, maombezini lakini hajawahi kukua kiroho yaani hana badiliko katika maisha yake; anakwenda kanisani kwa mazoea tu maana amekuta wanaomzunguka wanakwenda kanisani lakini hajui kwa nini hasa anakwenda kanisani.

 

Kwa jinsi yoyote ile ni vema kujiuliza, wewe msomaji mwanadamu unapokeaje neno la Mungu ambacho ndicho chakula cha Roho? Chakula ambacho kinarejesha afya ya roho na mwili, mafanikio ya kiroho na yakimwili, maendeleo ya kitumishi na kimaisha, badiliko yanayopelekea kukua kiroho, kuvunja nira kule ulikokamatwa na kuona kama ndiko sahihi, kukata kamba za uovu, kuachiwa huru kwa walioonewa, kuangusha ngome na kadhalika?

 

Mama huyu baada ya kumchunguza niligundua alikuwa ni “Nafsi mfu.” Niliamua kumfundisha mama huyu somo la NAFSI. Somo hili la Nafsi mfundishaji akifundisha kiusahihi anayefundishwa hupokea Baraka za ajabu na hata kuuona uthamani wake tena! Nafsi inaweza kuibwa,kutekwa,kufungiwa,kuzikwa,kutumikishwa na kadhalika.

 

Mambo yaliyotokea:

Kufunguliwa kwa Nafsi. Nafsi  ilipofungwa, ufahamu ambao muda mrefu ulifungwa ulifunguliwa. Mama alikua kiroho. Kumbuka ndugu msomaji kuwa nafsi ikifungwa hata maisha ya mtu kwa sehemu kubwa huwekwa njia panda, sababu nguvu za mtu katika utendaji zimeshikwa kule kwenye nafsi yake.

 

Mfano hai ni huyu mama ambaye kwa miaka kumi na nane alikuwa hajawahi kupata kazi, ambapo alikuwa akitunzwa na mumewe… sasa amepata kazi, ikiwa ni pamoja na kujiajiri mwenyewe! Alikuwa na kiwanja ambacho hakijawahi kuleta badiliko lolote hapo awali, lakini sasa mpaka kitabu kinaenda mitamboni kaweka msingi wa nyumba ikiwa ni pamoja na kuingiza bomba la maji.

 

Kifungo hiki cha nafsi hakikumkamata yeye peke yake, ni mpaka katika familia. Watoto walikuwa na taabu ya ada shuleni ambapo lilikuwa kama janga la kifamilia, lakini baada ya kufunguliwa upande ule wa nafsi tatizo likaisha mpaka katika kusomesha; watoto wanasoma vizuri sasa tofauti na zamani. Mama huyu kwa sasa amekuwa ni mtumishi wa Mungu ambaye analiishi neno la Mungu na Mungu akizidi kumkirimia mambo mema makuu ambayo hakupata kuyajua zamani hizo amen.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

KUKOMBOLEWA KATIKA NAFSI

NAFSI NI NINI?

Nafsi ndiye mtu kamili aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu. Ni wewe halisi, kwa lugha nyepesi ni mtu wa ndani asiyeonekana ambaye ndiye mwenye maamuzi yote juu ya maisha ya mwanadamu. Nafsi ina uwezo mkubwa kama kufunga ufahamu ama kuufungua. Kwa hakika nafsi yako na yangu zimebadili vitu vingi.

Nafsi imebadilisha maisha ya mwanadamu. Jinsi ulivyo sasa na misimamo na maamuzi yako vilivyopelekea ufanikiwe ama ushindwe vinatokana na nafsi ilivyofanya maamuzi huko nyuma na ikibidi inavyofanya maamuzi sasa. Hebu tuone machache kuhusu mifano ya nafsi kule inakofanyia kazi zake zinazodhihirishwa machoni ijapo nafsi yenyewe haionekani katika macho:-

i.                    Katika Maisha

ii.                  Katika Kazi

iii.                Katika Biashara

iv.                 Katika Familia

v.                   Katika Maisha ya ndoa

Matokeo ama niseme mwelekeo wa vitu vyote nilivyoviorodhesha hapo juu, bila shaka vinahusu nafsi. Hebu tuone mtu ili awe mtu lazima awe na mambo haya matatu au  vitu hivi vitatu  kama kielelezo kinavyoelezea hapa chini:

 

Aina Mbili za NAFSI

1. Nafsi mfu

2. Nafsi hai                                

 

 

Ziko aina mbili za nafsi, katika hizo lazima mojawapo iwe kwa mtu. Haiwezi kutokea mtu mmoja akawa na zote mbili. Kwa nini haiwezekani? Kwa sababu ya ule mfano usemao nuru na giza haviwezi kukaa pamoja, kila penye nuru giza halitakuwepo na palipo na kiza ni wazi nuru haipo. Aina hizi mbili za nafsi zinajibu hoja na mfano huu kuwa kila palipo na dhambi maana yake ni kuwa hakuna utakatifu na vivyo hivyo palipo na utakatifu uovu haukai.

Lakini katika hoja ya utakatifu na dhambi, dhambi inaruhusu mchanganyo, lakini utakatifu unataka kujitegemea wakati wote. Haya tuzione aina hizi mbili:-

 

 

1.      Nafsi Mfu: Nafsi mfu ni nafsi ya mtu aliyefungwa (ufahamu). Mtu mwenye nafsi hii anaweza akawa na bidii ya kuhudhuria ibadani kila wakati lakini hajawahi kukua kiroho, hana badiliko katika maisha yake na hawezi kuwa na mabadiliko kamwe. Anakwenda kanisani kwa mazoea lakini hana neno la Mungu hata chembe moyoni mwake. Huyu ni mfu, mtu wa ndani ameshakufa; mtu huyu wa ndani ndiye anayeitwa nafsi hai.

 


NAFSI MFU HII                                                                             

                                                                                               ROHO

                                                                                                              NAFSI

                                                                                                              MWILI

 

 

 

(HAJUI CHOCHOTE YUPO KATIKA UTUMWA)

2.  Nafsi Hai: Nafsi ni mtu aliyebadilishwa maisha na Yesu. Tunamwita kiumbe kipya, yaani kazaliwa upya. Mpendwa msomaji, uhai wa nafsi ni suala la kiimani kwamba mtu kapata neema ya kuhubiriwa Neno kwa njia yoyote ile iwe ni kwa ushuhuda-kashuhudiwa, au kahubiriwa, ama kafundishwa! Uhai ni ile hali ya kutambuliwa na Mungu kuwa mtu yu salama katika maisha ya sasa na yale yajayo, tunaita maisha ya milele!

 

 

 


                                         

3.

 

                                                                        

 

Comments

Popular posts from this blog

maombi